Katika pita pita zetu za Mtaa kwa Mtaa,tuliibuka maeneo ya Tabata Matumbi jijini Dar es Salaam na kukutana na mziki huu mnene na wakutatanisha uliozikutanisha gari mbili,ukiangaliwa kwa makini utabaini kuwa hili gari kubwa lenye nambari za Usajili T 544 CKG mali ya Kampuni ya Azania lilikuwa lipo kwenye njia yake halali kabisa kuelekea Buguruni na huyo mwenye Gari ndogo lenye nambari za Usajili T806 AVT anaonekana akielekea Ubungo lakini katika njia ambayo haimruhusu yeye kupita.Kilichotokea hapo ndio kama inavyoonekana pichani.Sasa sijui huyo mwenye hiyo gari ndogo alijiona anaendesha Boda boda....!!! Maana hapo alipotaka kupita hata hapaelezeki.
 Hapa hata sijui walitaka kupishana vipi??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Huu mwengine ni wazimu ulioongezewa bangi.

    Mtu kama huyu ni wa kunyang'anywa leseni angalau kwa mwaka mmoja ili ajirekebishe.

    ReplyDelete
  2. Hapa Tanzania ninaweza kupata leseni kwa muda wa masaa mawili. Na ninaweza kukutafutia leseni halali hata kama hujui kuendesha. Wewe tayarisha tu fungu la kutosha. Hii ni Bongoland. Ndivyo tunavyokula hapa. Mambo ya kunyanganywa leseni ni ya huko nchi za nje. Hapa hakuna system. Wewe unaona kashfa za mabilioni kwa wakubwa, unadhani sisi wadogo tunaishije. Mimi ninawaomba mlio nje mrudi mje mtusaidie kurekebisha system hapa. Vinginevyo hapa tunaishi kwa sheria za porini. Survival of the fitest.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...