Katibu mpya wa Yanga Dk. Jonas Tiboroha, ametangaza mikakati yake ya kuhakikisha Yanga inajiendesha kiuchumi ikiwa ni pamoja na kupitia upya mikataba yote ya wadhamini.
Akizungumza Makao Makuu ya Klabu hiyo leo, Tiboraha alisema kuwa Yanga ni klabu kubwa hiyo ni wakati wa kujiendesha yenyewe badala ya kutegemea mtu binafsi na kwamba haiwezi kuwa na mikataba ambayo haikithi maslahi ya klabu hiyo.
"Yanga ni bidhaa inayojiunza yenyewe uwezi kuingia mkataba wake sawa na Stand United, haiwezekani ikapata mgao sawa kama wanafunzi wa shule ya msingi unawapanga mstari unawambia haya kila mtu unamgawia pipi moja moja na wanaridhika, haiwezekani ni lazima Yanga iwe tofauti.
"Klabu kama Liverpol, inawashabiki wengi hata kama haipo kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi linapokuja suala la mgao wa fedha inapata fungu kubwa kwa vile tayar inajiuza, sasa Yanga ingie mikataba sawa na kina Stand United dunia nzima itatushangaa."alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...