Katibu Mkuu wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Ndugu Sixtus Mapunda anategemea kufanya ziara ya siku kumi na nne (14) katika mikoa minne ya Kanda ya Ziwa, ambayo ni Tabora, Shinyanga, Geita na Kagera kuanzia kesho tarehe 12 Dec 2014.

Ziara hii ya kikazi ya Katibu Mkuu inalenga kukagua na kuhimiza ujenzi na uimara wa jumuia ya Vijana katika maeneo husika lakini pia kushiriki kampeni zinazoendelea za uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 14th Dec 2014.

Pia, Katibu Mkuu anatarajia kufanya mikutano ya ndani na viongozi wa Jumuiya na Chama, pia kufanya mikutano ya hadhara inayolenga kuingiza wanachama wapya ndani ya jumuiya na chama kwa ujumla.

Kuhimiza wanachama wa chama cha mapinduzi na viongozi kuwaandaa wananchi katika kuipigia kura katiba mpya iliyopendekezwa wakati ukifika.

Ziara hiyo ya Katibu Mkuu inategemea kumalizika tarehe 25th Dec 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...