Mahakama moja nchini Kenya imeiamuru serikali kutoa hati ya kuzaliwa kwa mtoto wa umri wa miaka mitano aliyezaliwa akiwa na jinsia za kike na kiume. 

Wakati alipozaliwa mtoto huyo, wafanyakazi wa hospitali waliweka alama ya kuuliza penye kisanduku cha jinsia kwenye fomu ya uzazi mwaka 2009 baada ya kushindwa kuamua kama ni wa kike ama wa kiume.
Wakili wa mtoto huyo ameeleza kufurahishwa na hukumu hiyo akisema ni hatua moja kwenda mbele katika kutambua watu wenye jinsia mbili wanaojulikana kitaalamu kama "Intersex persons".
Hukumu hiyo inamaanisha kwamba sasa mtoto huyo atapatiwa cheti cha kuzaliwa kitachomuwezesha kufaidi haki zake zote za msingi kama vile elimu, kupata kitambulisho cha Taifa na kupiga kura. "Sasa watampatia mtoto huyu cheti cha kuzaliwa", alisema wakili wake Bw. John Chigiti. "Huu ni ushindi..."
Watu wenye jinsia mbili wamekuwa wakinyanyapaliwa maana hali hiyo haieleweki, ambapo wengi huiita ni "Mkosi".Mahakama hiyo pia ilimuamuru Mwanasheria Mkuu kuunda chombo kitakachokuwa na jukumu la kufanya sensa ya watu wenye jinsia mbili na kutengeneza kanuni na sera kwa ajili ya kutambulika kwao na usaidizi."Hakika uamuzi huo unatia moyo sana kwa sababu kama kanuni zinatengenezwa hii ina maana kuwa watu wa aina hii watatambulika rasmi". alisema Wakili Chigiti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...