MWANAMUZIKI mkongwe pia Kiongozi wa bendi ya Twanga Pepeta Luizer Mbutu amesema katika kupamba usiku wa Luizer Mbutu ikiwa ni maadhimisho ya miaka 16 ndani ya bendi bila kutoka ataimba nyimbo zote za bendi ambazo alishiriki kwa namna moja ama nyingine.

Akizungumza na Ripota wetu jana Mbutu alizitaja baadhi ya nyimbo hizo kuwa ni ‘Kisa Cha Mpemba’, ‘Jirani’, ‘Fainali Uzeeni’, ‘Mtu Pesa’, ‘Safari 2005’, ‘Mwana Dar es Salaam’ , ‘Kuolewa’ pia kutakuwa na wimbo maalum siku hiyo.

Mbutu aliongeza kwa kusema kuwa amefurahishwa na wasanii wa kike kujitokeza katika kutoa sapoti siku hiyo ambapo anamtaja mwanamuziki aliyeongezeka kuwa ni Hafsa Kazinja, ambaye atajumuika na Stara Thomas ‘Stara T’, Siza Mazongera ‘Mamaa wa Segere’.

Wengine ambao watanogesha onyesho hilo kuwa ni bendi ya Utalii inayoongozwa na Komandoo Hamza Kalala ‘Mzee wa Mdaongo’, bendi ya Msondo Ngoma .

Wakati huohuo Mbutu alisema kwamba naye waliokuwa wanenguaji wakali wa bendi ya hiyo Lilian Tungaraza ‘Lily Internet’ na Aisha Madinda nao watakuwepo siku hiyo ambapo wataudhihirishia umma kwamba bado wako gado.

Mbutu alisema kwamba pia mwanamuziki ambaye aliwahi kufanya kazi katika bendi hiyo Roggert Hegga ‘Caterpiller’ , Bob Gaddy Wai na Ramadhan Masanja wamethibitisha kuwepo katika maadhimisho hayo yatakayofanyika Desemba 20 katika ukumbi wa Mango Garden Kindoni Jijini Dar es Salaam kwa kiingilio cha sh.10,000.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Asha Baraka alisema kuwa wameandaa onyesho hilo ambalo litakua maalum kwa Kiongozi wa bendi hiyo ambaye anaetimiza miaka 16 ndani ya bendi bila kuhama tangu ilipoanzishwa hivyo wanafanya hayo ikiwa ni katika kuenzi mchango wake ndani ya bendi.

“Uongozi wa ASET umeamua kuandaa usiku maalum wa kumuenzi Luiza kutokana na kua na msimamamo wa kukaa katika bendi kwa muda wote huo bila kuhama hilo ni jambo la kujivunia” alisema Mkurugenzi wa bendi Asha Baraka.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa wao kama ASET wanatambua mchango wa Luiza ndani ya bendi hiyo hivyo kutakuwa na tukio la aina yake ambalo mashabiki na wadau wa bendi hiyo pamoja na wapenzi wa Luiza wajitokeze kwa wingi siku hiyo kushuhudia litakalojiri sambamba na kupata burudani kutoka kwa bendi ya Twanga Pepeta.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...