Na Ripota Wetu,Dar 

MASTAA nane wa klabu ya Msimbazi wamekacha timu hiyo iliyoandoka leo kwenda Zanzibar kwa kile wanachoshinikiza kulipwa fedha zao. Habari za kuaminika zinasema kuwa mastaa nane wa klabu hiyo wameingia mitini wakiwemo waganda watano na wabongo watatu mpaka hapo watakapomaliziwa fedha zao za usajili.

Wabongo waliokacha timu hiyo ni Shaban Kisiga, Jonas Mkude na Ivo Mapunda hata hivyo kocha msaidizi wa timu hiyo Seleman Matola jana alikiri kutokuwepo kwenye kikosi chake wachezaji hao na kuweka wazi kuwa Ivo amekwenda Mbeya kwenye arobaini ya mama yake mzazi aliyefariki hivi karibuni, huku akiwa hana taarifa za Kisiga na Mkude.

Pia mbali na wachezaji hao wa kibongo, wachezaji waganda ambao wameingia mitini ni Emmanuel Okwi ambaye alikuwa wa kwanza kutimka mara baada ya kichapo cha bao 1-0 dhidi ya Kagara. Wengine ni Joseph Owino, Dan Sserunkuma, Juuko Murshid na Simon Sserunkuma.

"Ninaondoka na wachezaji wachache, nina taarifa za Ivo tu ambaye ameenda kwenye harobaini ya mama yake, wengine sina taarifa zao." alisema Matola ambaye hata hivyo ameaidi kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi.

Kikosi hicho cha Simba kimeondoka leo asubuhi kuelekea Zanzibar tayari kwa michuano ya Kombe la Mapinduzi itakayoanza kutimua vumbi keshoJanuari Mosi hadi Januari 13 kwenye uwanja wa Aman visiwani Zanzibar.

Mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hanspope alipotafutwa kuzungumzia suala hilo alisema kwa kifupi "Nipo Iringa, sijui chochote kinachoendelea Simba kwa sasa, hayo mambo waulizeni viongozi waliopo huko, mi mwenyewe nasikia tu lakini sijui chochote."

Mwenyekiti wa Simba Evans Aveva hakupatikana kuzungumzia suala hilo, hata hivyo mmoja wa viongozi wa klabu hiyo aliiambia Mwananchi kuwa wachezaji hao waliondoka kwa vile Simba hawakuwa na uhakika wa kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi.

"Unajua barua ya kuthibitisha yenyewe imetumwa juzi tu, hatukuwa na uhakika wa kushiriki ndio maana tuliwaruhusu wachezaji kuondoka na warudi tarehe moja, wote wana ruhusa maalum."alisema mmoja wa viongozi wa wekundu hao wa Msimbazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...