Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akimkabidhi cheti mmoja ya washiriki wa mafunzo ya D.H.I.S  Osama Al Zubair  kutoka Sudan wakati wa kufunga mafunzo hayo katika Hoteli ya Double Tree Nungwi, Kaskazini Unguja.
 Mgeni rasmi katika ufungaji wa mafunzo ya D.H.I.S Mahmoud Thabit Kombo akiwahutubia washiriki wa mafunzo hayo kutoka Nchi za Afrika, Marekani, Ujerumani na Mashirika wahisani katika Hoteli ya Double Tree Nungwi.
 Mratibu wa mafunzo ya mfumo wa ukusanyaji taarifa za Afya (D.H.I.S) Suleiman Salum  Ali  akieleza mafanikio  ya mafunzo hayo  yaliyofanyika Hoteli ya Double Tree Nungwi, wa kwanza (kulia) ni Profesa Kristin Braa kutoka Chuo Kikuu cha Oslo ambao ni waandaaji wa mafunzo hayo kwa kushirikiana  na Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Wizara ya Afya Zanzibar. (kati) ni Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo aliefunga mafunzo hayo. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo zanzibar)
 Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo alipokuwa akiyafunga mafunzo ya siku 10 yaliyofanyika Hoteli ya Double Tree Nungwi.
 Mratibu wa mafunzo ya mfumo wa ukusanyaji taarifa za Afya Suleiman Salum Ali akizungumza na waandishi wa Habari walioshiriki ufungaji wa mafunzo hayo katika Hoteli ya Double Tree Nungwi.
 Picha ya pamoja ya washiriki wa mafunzo ya mfumo wa ukusanyaji taarifa za Afya (D.H.I.S) wakiwa na mgeni rasmi katika kufunga mafunzo hayo Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo katika Hoteli ya Double Tree Nungwi. (Picha na Makame Mshenga-Maelezo zanzibar).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...