Benki ya NMB kwa kuelewa uhitaji wa vifaa vya hospitali na madawati katika jamii
inayoizunguka, imetoa vifaa vya hospitali vyenye thamani ya shilingi milioni tano kwa
ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Nanyumbu pamoja na madawati sabini yenye thamani ya
shilingi millioni tano kwa Shule ya Msingi Likokona iliyoko Wilayani Nanyumbu, Mkoani
Mtwara.
Msaada huo uliopokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga, ni
mwendelezo wa sera ya NMB ya kuchangia huduma za jamii ili kukabiliana na
changamoto zinazokabili sekta ya elimu na Afya.
Akitoa shukrani kwa niaba ya wakazi wa Nanyumbu.Mhe Kiswaga alisema “Msaada huu
ambao tumeupokea leo kutoka NMB, utasaidia kupunguza uhaba mkubwa tuliokua nao
kwa kipindi kirefu. Vifaa tiba vimekua havitoshelezi katika hospitali yetu lakini pia
madawati nayo imekua ni kilio kikubwa katika shule za hapa Nanyumbu. Lakini leo NMB
wamekua sehemu ya maisha yetu na hivyo wameweza kujua hitaji letu na kutusaidia.
Naomba kutoa shukrani za pekee kwa uongozi mzima wa NMB.
Meneja wa kitengo cha biashara za Serikali wa NMB Kanda ya Kusini ,Mr.Haji Msigwa akimkabidhi
vifaa vya Hospitali Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga kwa ajili ya Hospitali ya
Wilaya ya Nanyumbu.
Meneja wa kitengo cha biashara za Serikali wa NMB Kanda ya Kusini, Mr. Haji Msigwa akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga sehemu ya madawati yaliyotolewa kwa ajili ya Shule ya Msingi Likokona .
Wanafunzi wa shule ya msingi Likokona walioshiriki hafla ya makabidhiano
Sehemu ya Madawati yaliyotolewa na NMB.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...