Benki ya NMB kwa kuelewa uhitaji wa vifaa vya hospitali na madawati katika jamii inayoizunguka, imetoa vifaa vya hospitali vyenye thamani ya shilingi milioni tano kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Nanyumbu pamoja na madawati sabini yenye thamani ya shilingi millioni tano kwa Shule ya Msingi Likokona iliyoko Wilayani Nanyumbu, Mkoani Mtwara.

Msaada huo uliopokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga,   ni mwendelezo wa sera ya NMB ya kuchangia huduma za jamii ili kukabiliana na changamoto zinazokabili sekta ya elimu na Afya.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wakazi wa Nanyumbu.Mhe Kiswaga alisema “Msaada huu ambao tumeupokea leo kutoka NMB, utasaidia kupunguza uhaba mkubwa tuliokua nao kwa kipindi kirefu. Vifaa tiba vimekua havitoshelezi katika hospitali yetu lakini pia madawati nayo imekua ni kilio kikubwa katika shule za hapa Nanyumbu. Lakini leo NMB wamekua sehemu ya maisha yetu na hivyo wameweza kujua hitaji letu na kutusaidia. Naomba kutoa shukrani za pekee kwa uongozi mzima wa NMB.
Meneja wa kitengo cha biashara za Serikali wa NMB Kanda ya Kusini ,Mr.Haji Msigwa akimkabidhi vifaa vya Hospitali   Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Nanyumbu.
Meneja wa kitengo cha biashara za Serikali wa NMB Kanda ya Kusini, Mr. Haji Msigwa akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe. Festo Kiswaga  sehemu ya madawati yaliyotolewa kwa ajili ya Shule ya Msingi Likokona .
Wanafunzi wa shule ya msingi Likokona walioshiriki hafla ya makabidhiano
Sehemu ya Madawati yaliyotolewa na NMB.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...