Benki ya NMB leo imefungua tawi jipya maeneo ya Gongo la mboto- Dar es Salaam tawi linalokadiriwa kuhudumia zaidi ya wateja 300 kwa siku. Tawi hili lipo karibu na kituo cha dala dala cha Mzambarauni mkabala na kituo cha mafuta Oil com.

Tawi hili linatoa huduma kwa wakazi wa Chanika,Pugu,Majohe,Kitunda,Mongo la ndege na maeneo yote ya karibu.Vile vile huduma zote za kibenki zinapatikana katika tawi hili zikiwamo ufunguzi wa akaunti mbali mbali,Huduma za mikopo pamoja na huduma za kuweka na kutoa fedha.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Mhe. Raymond Mushi, akikata utepe kuashiria  uzinduzi rasmi wa tawi la NMB Gongo la Mboto .  Kushoto  ni Meneja wa NMB Kanda ya Dar e salaam – Bw. Salie Mlay  na  kulia ni  meneja wa NMB Tawi la Airport Bi.Hellen Mapunda.
Mhe.Raymond Mushi akiongea na sehemu ya wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Tawi.
Mhe. Raymond Mushi akiwa kwenye picha ya pamoja na maofisa wa NMB mara baada ya uzinduzi rasmi wa tawi la Gongo la Mboto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. SAFI SANA, TUNAOMBA NA KIMARA MWISHO MTUFUNGULIE TAWI, TUNAPATA SHIDA SANA MPAKA TUENDE MLIMANI CITY, JAMANI TUSAIDIENI. MKIFUNGUA KIMARA INA MAANA MBEZI, BONYOKWA, KING'ONGO, MATOSA, GOBA, MSUMI, MALAMBAMAWILI, KIBAMBA WOTE WATAPATA HUDUMA KIMARA, MAANA KITUO KIKUBWA KITAKUWA NI KIMARA MWISHO. TUSAIDIENI WADAU.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...