
Wakati
huo huo , Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira, Dkt. Binilith Mahenge amewateua Wajumbe wa Bodi hiyo .
Walioteuliwa ni Profesa Reuben
Mwamakimbulah kutoka Chuo kikuu cha Sokoine Morogoro, kitivo cha Misitu na Utunzaji wa mazingira,
Injinia Bengiel Humphrey Msofe ambaye
ni Mkurugenzi wa huduma za ufundi kutoka Wizara ya Nishati na Madini , Bi Judica
Haikase Kida Omari, Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya fedha na Uchumi.
Wajumbe
wengine walioteuliwa ni Injinia Frida Rweyemamu, Mkuu wa Idara ya maji vijijini
kutoka Wizara ya Maji, Ndugu Sheha Mjaja Juma
Mkurugenzi Idara ya Mazingira kutoka
Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Juma Mgoo ambaye ni
Mkurugenzi Mtendaji Wakala wa
Misitu Tanzania (TFS) kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii , Bi Anna William
Mtani, Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya
Miji kutoka Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI).
Mwingine ni Julius Keneth Ningu kutoka Ofisi
ya Makamu wa Rais yeye ni Mkurugenzi Idara
ya Mazingira . Uteuzi huo unaanza rasmi tarehe
18/12/2014
Imetolewa na
KATIBU MKUU
OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...