Serikali kupitia Ofisi ya Waziri
Mkuu-TAMISEMI leo imetangaza kuwasimamisha kazi Wakurugenzi watano (5) huku
wengine wakipewa onyo kali katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akithibitisha kusimamishwa kazi kwa
Wakurugenzi hao,Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu,Mh. Hawa Ghasia amesema kwamba
Wakurugenzi hao wametenda makosa yanayowaondolea sifa za kuwa Wakurugenzi.
“Makosa yafuatayo ndio yanayopelekea
Wakurugenzi hawa kusimamishwa;Kuchelewa kuandaa vifaa vya kupiga kura,kukosa
umakini katika kuandaa vifaa hasa karatasi za kupigia kura,kuchelewa kupeleka
vifaa kwenye vituo vya kupigia kura,uzembe katika kutekeleza majukumu yao
pamoja na kutoa taarifa za kupotosha kuhusu maandalizi ya uchaguzi kuwa
yamekamilika huku wakijua kuwa siyo kweli”,alisema Ghasia
Aidha,Mh.Ghasia ameridhishwa na hatua ya
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala kumchukulia hatua mtumishi wake aliyemsingizia
Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali na kusema ni jambo baya kutenda kosa na kusingizia
watu au ofisi zisizohusika.
Wakurugenzi wanaosimamishwa kazi na kupisha
uchunguzi zaidi ni pamoja na
i)
Bw.Felix T.Mabula-Halmashauri
ya Hanang’
ii)
Bw.Fortunatus Fwema-
Halmashauri ya Mbulu
iii)
Bi.Isabela D.Chilumba- Halmashauri
ya Ulanga
iv)
Bi.Pendo Malabeja- Halmashauri
ya Kwimba
v)
Bw.William
Z.Shimweta-Sumbawanga Manispaa
Pia, Mh.Hawa Ghasia amesema Wakurugenzi wengine watatu(3)
wanapewa onyo kali na watakuwa chini ya uangalizi kubaini kama
wana udhaifu mwingine ili wachukuliwe hatua zaidi Wakurugenzi hao ni:-
i)
Bw.Mohamed A.Maje-Halmashauri ya Rombo
ii)
Bw.Hamis Yuna- Halmashauri ya
Busege
iii)
Bw.Jovin A.Jungu- Halmashauri
ya Muheza
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...