Baadhi ya wananchi wa wadau wa Afya wakifanya maandamano wakati wa Uzinduzi wa kampeni ya NYOTA YA KIJANI uliofanyika eneo la kumbukumbu ya Mwl.Nyerere Tabora mjini.
Mmoja kati ya maafisa kutoka Wizara ya Afya Bi.Isabela Nyalusi akisoma taarifa fupi ya hali ya matumizi ya Uzazi wa Mpango kwa kanda ya Magharibi ambapo inaonesha kuwa mikoa ya kanda ya magharibi ina kiwango kidogo cha utumiaji wa huduma za uzazi wa mpango kwa asilimia 19 ikilinganishwa na mikoa ya kanda ya kaskazini yenye asilimia 50.
Kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Tabora Dr.Fikiri Martine akizungumza katika uzinduzi wa Kampeni hiyo ambapo alieleza kuwa matumizi ya huduma ya uzazi wa mpango yameanza kupanda katika siku za hivi karibuni licha ya kuwa bado jamii imekuwa ikikabiliwa na dhana potofu juu ya mpango huo.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tabora mjini Bw.Suleiman Kumchaya akizungumza katika uzinduzi huo amewataka wananchi mkoani Tabora kuzitumia njia za uzazi wa mpango kwakuwa ni njia salama na zinazoweza kusaidia kupanga maisha katka mpangilio mzuri.
Kaimu mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Suleiman Kumchaya akikata utepe kama ishara ya Uzinduzi wa Kampeni ya Nyota ya kijani zoezi lililofanyika chini ya sanamu ya kumbukumbu ya Hayati Baba wa Taifa Mwl.Julius Nyerere mjini Tabora.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...