SHIRIKA
LA USAFIRI DAR ES SALAAM (UDA)
SHIRIKA la Usafiri Dar es Salaam (UDA)
linawatangazia Watanzania wote hususan wakazi wa jiji la Dar es Salaam kwamba
linahitaji kuajiri madereva kwa ajili ya
kuendesha mabasi yake hapa jijini.
SIFA
ZA WAOMBAJI
Waombaji wa kazi ya udereva wanatakiwa kuwa na umri
wa kuanzia miaka 30-55, ujuzi wa udereva wa mabasi kutoka katika vyuo vya VETA,
NIT, au chuo kingine kinachotambulika na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi nchini
(NECTA). Pia wanapaswa kuwa na leseni ya udereva daraja C Kavu (Class C Plain)
na daraja C1(Class C1) , rekodi nzuri ya utendaji na afya njema.
NAMNA
YA KUOMBA
Waombaji wote walete barua zao za maombi
wakiambatanisha na barua za udhamini, walete barua hizo kwa mkono katika Ofisi
ya Afisa Rasilimali watu na Utawala, Makao Makuu ya UDA, KAMATA COMPLEX, mahali
zilipokuwa ofisi za mabasi ya SCANDINAVIA.
Wanawake wanyesifa wanahimizwa zaidi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA NAMBA 255222127421,
0766777754, 0766777753 ,0754776700, 0715776500,0712000037 au wasiliana kwa
barua pepe info@uda.co.tz, uda@umojainvestments.com au kwa
sanduku la posta
Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA)
S.L.P 872
Dar Es Salaam,Tanzania
LIMETOLEWA
NA OFISI YA MAHUSIANO YA UMMA UDA
DESEMBA
01, 2014.
Please make sure that on top of all the other tests that will be run before confirming a position, that shortlisted candidates are given a drug test and have a background check done for each one. Also, a 6 month probation where drug / alcohol tests and urine samples are taken randomly without warning. After that, random drug, alcohol and eyesight tests should be conducted on a regular but random basis...spot checks method.
ReplyDelete