SHIRIKA LA USAFIRI DAR ES SALAAM (UDA)
 
SHIRIKA la Usafiri Dar es Salaam (UDA) linawatangazia Watanzania wote hususan wakazi wa jiji la Dar es Salaam kwamba linahitaji kuajiri madereva  kwa ajili ya kuendesha mabasi yake hapa jijini.
 
SIFA ZA WAOMBAJI
Waombaji wa kazi ya udereva wanatakiwa kuwa na umri wa kuanzia miaka 30-55, ujuzi wa udereva wa mabasi kutoka katika vyuo vya VETA, NIT, au chuo kingine kinachotambulika na Mamlaka ya Elimu ya Ufundi nchini (NECTA). Pia wanapaswa kuwa na leseni ya udereva daraja C Kavu (Class C Plain) na daraja C1(Class C1) , rekodi nzuri ya utendaji na afya njema.
 
NAMNA YA KUOMBA
Waombaji wote walete barua zao za maombi wakiambatanisha na barua za udhamini, walete barua hizo kwa mkono katika Ofisi ya Afisa Rasilimali watu na Utawala, Makao Makuu ya UDA, KAMATA COMPLEX, mahali zilipokuwa ofisi za mabasi ya SCANDINAVIA.
 
Wanawake wanyesifa wanahimizwa zaidi.
KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA NAMBA 255222127421, 0766777754, 0766777753 ,0754776700, 0715776500,0712000037 au wasiliana kwa barua pepe info@uda.co.tz, uda@umojainvestments.com au kwa sanduku la posta
Shirika la Usafiri Dar Es Salaam (UDA)
S.L.P 872
Dar Es Salaam,Tanzania
LIMETOLEWA NA OFISI YA MAHUSIANO YA UMMA UDA

DESEMBA 01, 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Please make sure that on top of all the other tests that will be run before confirming a position, that shortlisted candidates are given a drug test and have a background check done for each one. Also, a 6 month probation where drug / alcohol tests and urine samples are taken randomly without warning. After that, random drug, alcohol and eyesight tests should be conducted on a regular but random basis...spot checks method.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...