Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Fanuel Mbonde akijaribu baiskeli ya mazoezi aliyokabiodhiwa kama zawadi katika hafla ya kuwapongeza watumishi wa Wizara waliostaafu iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki na kulia ni Katibu Mkuu Bi. Maimuna Tarishi.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Angellah Kairuki (kushoto) akimkabidhi zawadi Mtunza Kumbukumbu Mstaafu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bi. Clara Mlamlyingu katika hafla ya kuwapongeza watumishi wa Wizara waliostaafu iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Bi. Mlamlyingu ni Katibu Mkuu Bi. Maimuna Tarishi na kulia ni Jaji Dkt. Gerrald Ndika, Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania.
Watumishi Wastaafu wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa na vyeti vyao katika picha ya kumbukumbu na viongozi wa Wizara wakiongozwa na Naibu Waziri Mhe. Angellah Kairuki na Katibu Mkuu Bi. Maimuna Tarishi. Hafla ya kuwapongeza ilifanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...