Pichani juu ni sehemu ya kipande cha barabara ya lami ambacho tayari kimekwisha kamilika,kama kilivyonaswa na Globu ya Jamii wakati ikivinjari katika barabara hiyo jana na kujionea ujenzi huo ukienda kwa kasi,barabara hiyo ambayo imeonekana kuwa na umuhimu mkubwa katika jitihada za kupambana na msongamano wa magari ambao umekuwa kero kubwa kwa wakazi wa jiji la Dar na kwingineko.Barabara hiyo almaarufu kwa jina la barabara ya chuo kikuu ambayo pia unaweza kwenda Goba ama kuchepuka na kutokea Mbezi ya kimara na kuendelea na safari yako,kwa sasa aghalabu inapitika kwa kiasi kikubwa.
Home
Unlabelled
UJENZI WA BARABARA YA CHUO KIKUU KUTOKEA MBEZI YA KIMARA UKIENDELEA KWA KASI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Na bado kuna wanaoibeza Serikali ya CCM? Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
ReplyDeleteArdhi-Makongo-Goba kulikoni? Tuliambiwa toka mwaka juzi iko katika plan kuwekwa lami.
ReplyDelete