Ujumbe wa wataalamu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania ( TPA) unatembelea Bandari ya Singapore (PSA) ili kubadilishana utaalamu wa namna ha kuongeza ufanisi na kuimarisha Ulinzi na usalama wa Bandari kwa kutumia Mitambo ya kisasa na Teknolojia ya Habari na mawasiliano (ICT) , Ujumbe wa TPA unaongozwa na Ndg. Phares Magesa , Mkurugenzi wa ICT wa TPA, pia wamo wahandisi wa majengo, wataalamu wa Ulinzi na wataalamu wa  TEHAMA. Ziara hii ni muendelezo wa ushirikiano wa PSA na TPA ikiwa ni sehemu ya makubaliano yaliyotiwa sahihi kati ya TPA na PSA wakati wa ziara ya Mhe. Rais Kikwete alipotembelea nchini Singapore mwaka jana.
  Ujumbe wa TPA ulipotembelea eneo la Bandari ya Singapore linalotumika kwa ajili ya Meli za abiria, starehe na kuvinjari ( waterfront development ). 
 Ujumbe wa TPA ukiwa kwenye chakula Cha pamoja na Ujumbe PSA
 Ujumbe wa TPA ukiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa PSA makao makuu ya PSA
 Mkuu wa msafara Ndg. Magesa akisalimiana na Makamu wa Rais Msaidizi wa PSA anayeshugulikia ICT Ndg. Andrew Gill wakati akiwakaribisha makao makuu wa PSA
Mkuu wa msafira wa TPA Ndg. Magesa akipokea zawadi toka Makamu wa Rais Msaidizi wa Mamlaka ya Bandari ya Singapore ( PSA) anayeshugulikia biashara Ndg. Vignes kulia

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...