Na Andrew Chale
USIKU wa ‘Old
Is Gold’ na Spice Modern Taarab, unatarajiwa kurindima usiku wa
Desemba 28, Mwaka huu ndani ya ukumbi wa Safari Carnival
uliopo Mikocheni B, jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa
Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia Idarous Khamsin, mwandaaji na mdhamini wa
onyesho hilo, mashabiki wa Old Is Gold watapata
burudani ya aina yake katika kiota hicho cha burudani kila jumapili
kukumbushana enzi.
“Kwa kiingilio
cha sh 5,000 tu, wadau watafurahia shoo kabambe kutoka kwa Spice Modern Taarab
ndani ukumbi wa Safari Carnival. Huku wadau wakijumuika pamoja na kubadilishna
mawazo” alisema Asia Idarous.
Asia Idarous
alilielezea kundi hilo ni la magwiji wa muziki huo wa mwambao ikiwemo kupiga
nyimbo za taarab za zamani na zile za sasa.
Onyesho ni
la kila siku za Jumapili kwenye ukumbi huo huku likidhaminiwa na Fabak Fashions
(Mikocheni), Safari Carnival, wadau wengine wakiwa ni pamoja na
Clouds tv, Michuzi Media Group na wengine wengi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...