Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imeshirikiana na Timu ya mpira wa miguu ya Sunderland ya Uingereza katika uzinduzi wa utangazaji utalii wa Tanzania pamoja na uhamasishaji wa uwekezaji na maendeleo ya michezo (Destination Partner in Tourism and Sports Development). 
Uzinduzi huo ulifanyika tarehe 29 Novemba, 2014 kwenye kiwanja cha “Stadium of Light”, kinachomilikiwa na Sunderland Association Football Club (SAFC).
Tukio hilo lilihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Balozi Peter Kallaghe, Maafisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza, Watanzania waishio nchini Uingereza pamoja na baadhi ya maafisa wa Bodi ya Utalii Tanzania.
Wakati wa uzinduzi huo katika kingo za kuta za uwanja yalionekana matangazo yanayotangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ambapo kulikuwa na mechi kati ya timu ya Sunderland na Chelsea FC iliyorushwa moja kwa moja na kituo kinachorusha mechi mbalimbali za mpira wa miguu cha DSTV. Aidha wachezaji wa timu ya Sunderland walionekana wakiwa wamevaa jezi maalum  zilizoandikwa ‘Visit Tanzania’ wakati wakifanya mazoezi kabla ya mechi hiyo.
Bodi ya Utalii Tanzania imetumia fursa ya mechi hiyo kuhamasisha wageni mashuhuri kutoka ndani na nje ya Uingereza pamoja na mashabiki wa Timu hizo wa nchi zote duniani kutembelea vivutio vya utalii wa Tanzania.

Imetolewa na
BODI YA UTALII TANZANI

01/12/2014

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...