Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angellah Kairuki akihutubua katika mahafali ya 14 ya Chuo cha Uongozi wa Mahakama - Lushoto wilayani Lushoto hivi karibuni.

Wahitimu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama – Lushoto (IJA) wameaswa kutumia elimu waliyopata kwa kuwatumikia wananchi kwa uaminifu ili kulinda heshima ya chuo hicho.

Akizungumza hivi karibuni katika mahafali ya 14 ya chuo hicho yaliyofanyika wilayani Lushoto mkoani Tanga, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mheshiwa Angellah Kairuki aliwakumbusha wahitimu hao kuwa waaminifu na kulinda maslahi ya umma popote watakapobahatika kufanya kazi.

“Nitumie fursa hii kuwaasa sana wahitimu kwamba, popote mtakapobahatika kupata kufanya kazi, fanyeni kazi kwa umahiri mkubwa na kwa uaminifu, kwa wakati na kulinda maslahi ya umma wa Tanzania na hivyo kubeba taswira nzuri ya Chuo ipasavyo,” alisema Naibu Waziri Kairuki katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chuo hicho wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo, Jaji Mstaafu John Mrosso.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...