Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu wawili wakazi wa mkoa wa
Morogoro kwa tuhuma za kupatikana na magunia 12 ya Bangi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa
Polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na
askari waliokuwa doria.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea huko Desemba 2 mwaka huu
majira ya 4.40 usiku kwenye pori la Vikawe kata Pangani wilaya ya Kibaha.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Sabas Petro (25) na Emily Magomba (21)
ambao walikamatwa na askari waliokuwa doria.
“Watuhumiwa walikutwa wakishusha magunia hayo kwenye pori hilo kwa lengo la
kuyaficha kutoka kwenye gari namba T 773 ELB,” alisema Kamanda Matei.
Bange dawa....kamata escrow bwana aghh!
ReplyDelete