Na John Gagarini, Kibaha 

 JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu wawili wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa tuhuma za kupatikana na magunia 12 ya Bangi. 

 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa Polisi mkoani humo Ulrich Matei alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na askari waliokuwa doria. 

 Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea huko Desemba 2 mwaka huu majira ya 4.40 usiku kwenye pori la Vikawe kata Pangani wilaya ya Kibaha. 

 Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Sabas Petro (25) na Emily Magomba (21) ambao walikamatwa na askari waliokuwa doria. 

 “Watuhumiwa walikutwa wakishusha magunia hayo kwenye pori hilo kwa lengo la kuyaficha kutoka kwenye gari namba T 773 ELB,” alisema Kamanda Matei.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Bange dawa....kamata escrow bwana aghh!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...