Taarifa iliyoifikia Globu ya Jamii asubuhi hii,inaeleza kuwa majambazi yamevamia kituo cha Polisi cha Ikwiriri, Rufiji mkoani Pwani na kuua Askari wawili na kupora silaha (bunduki) zilizokuwepo kituoni hapo.
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo,huku askari wanaodaiwa kupotenza maisha ni Cop. Edgar aliyekatwa mapanga na Wp Judith aliyepigwa risasi ubavuni upande wa kulia na kutokea upande wa kushoto.
Hivi sasa hali ni tete katika eneo hilo na watu wamekusanyika huku polisi wakiongeza nguvu kusaka wauaji katika Tukio la uvamizi, kituo cha polisi Ikwiriri, Rufiji, Pwani
Silaha zilizoporwa ni SMG 2, SAR 2, SHORTGUN 1, silaha 2 za mabom ya machozi na risasi 60 za smg.
tutaendelea kujuzana kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia.
Mambo gani haya jamani. Wanaohusika wachukue hatua ili polisi wapewe usalama zaidi na matukio kama haya ya uvunjifu wa sheria na amani yasitokee tena.
ReplyDeleteKisha kuna wajinga wanatuambia eti tuondoshe hukumu ya kifo!!! Adhabu ya makosa kama haya itakuwa nini?
ReplyDeleteOccupational hazzard, Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi.
ReplyDeleteDuu hii mijambazi mi siipendi
ReplyDeleteKwanza Nawapa pole familia za marehemu kwa kufiwa na ndugu zao.
ReplyDeletePili, Watu wanatakiwa Wajiuzuru ndani ya jeshi la polisi maana huu ni uzembe mkubwa kwa kumbukumbu zangu inatokea mara mbili sasa baada ya ile ya Bukombe wakati huohuo tunasikia mara songea na Arusha milipuko...Kituo cha Polisi ni kama ngome ya kijeshi, inatakiwa ijiweke kikamilifu wakati wote dhidi ya mashambulizi na ukiona mashambulizi yanatokea mara kwa mara basi ujue kuna tatizo kwenye Chain of command ya kijeshi ktk vitengo vyao vyote...Jeshi imara ni lile linaloweza kuzuia tukio kabla halijatokea na inabidi wakati ufike kwa Tanzania kukubali kukosolewa ata kama hatupendi kusikia au kushauriwa na wahusika wajiuzuru na kukubari makosa.