Katibu Mkuu Ndugu Kinana sambamba na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Ujumbe wake ukipokelewa na vijana wa CCM jimbo la Donge wakiongozwa na Mbunge wao Mh.Sadifa Juma Khamis,mapema leo alipokuwa akiwasili kwenye ofisi za CCM-Donge Mtambalike wilaya ya Kaskazini B.Katibu Mkuu Ndugu Kinana yupo katika ziara ya Visiwa vya Unguja na Pemba-Zanzibar akihimiza Uhai wa chama cha CCM na kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010
 Pichani kulia ni Mbunge wa jimbo la Donge na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Taifa (UVCCM) ,Mh.Sadifa Juma Khamis akimpokea Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana pichani kati mara baada ya kuwasili katika jimbo hilo Wilaya ya Kaskazini B,mkoa wa Kaskazini B Unguja kwa ziara ya siku moja.Ndugu Kinana aliwasili katika ofisi za CCM Donge Mtambalike na kupokea taarifa ya chama ya wilaya na utekelezaji wa Ilani,na pia alizungumza na  Wajumbe wa Halmashauri kuu ya Wilaya.
 Mtunza fedha wa kikundi cha ushiriki cha akina Mama ,Saccos (kukopa na kuweka),Bi Mwatime Juma Omar akitoa ufafanuzi mfupi kuhusiana na ushirika huo kwa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pichani wa pili kushoto na Mbunge wa Jimbo la Donge,Mh.Sadifa Juma Khamis wakikabidhi mifuko ya saruji kwa Mwalimu Mkuu wa Skuli ya msingi ya Donge Mtambini,Bwa.Bakari Ame Hussein,Jumla ya mifuko  50 ya saruji ilitolewa na Mbunge Sadifa kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa skuli hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Makamu wa Pili wa Rais-Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd wakitazama shughuli mbalimbali za vijana wa Mafunzo ya Amali katika fani ya ushonaji.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia Wananchi na wafuasi wa CCM,katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Maskani ya CCM Kizota,jimbo la Kitope,Ndugu Kinana aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya kuipigia kura na Waipigie kura ya ndiyo Katiba inayopendekezwa kwa kuwa ina mambo mengi mazuri yenye faida kwa Wanzibari.
Mbunge wa Jimbo la Donge na Mwenyekiti wa Jumuia ya Vijana Taifa  (UVCCM),Ndugu Sadifa Juma Khamis akiwahutubia wananchi na wafuasi wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Maskani ya CCM Kizota,jimbo la Kitope.
Baadhi ya Wafuasi wa chama cha CCM,wakisikiliza yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Maskani ya CCM Kizota,jimbo la Kitope
Sehemu ya umati wa watu uliofika kwenye mkutano huo wa hadhara.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd mara baada ya mkutano wa hadhara kumalizika,shoto nyuma ya Balozi ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.

PICHA NA MICHUZI JR-MKOA WA KASKAZINI B-UNGUJA
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...