
WASOMAJI
na wadau wangu nawasalimu na naimani kuwa Mwenyezi Mungu ametujalia
tumeuona mwaka mpya wa 2015 salama salmini. Nawatakia heri na fanaka
katika mwaka huu pia na karibuni tena katika porojo zangu za ukweli.
IDARA ya
Habari –MAELEZO ndiyo idara ya serikali inayoshughulika na kufanya kazi zake
kama chombo cha usimamizi wa vyombo vya habari na waandishi wake.
Idara
hiyo pia ndio msemaji wa masuala mbalimbali ya serikali lakini pia ndiyo idara yenye
jukumu la kusajili au hata kuyafutia usajili magazeti hapa nchini na vyombo
mbali mbali vya hjabari.
Waandishi
wa habari waajiriwa na wale wa kujitegemea wameanza mchakato wa kujaza fomu
kwa ajili ya kupatiwa vitambulisho vipya vya kazi (PRESS CARD) kwa mwaka 2015.
Jambo
hili ni zuri kwa waandishi wa habari maana kitambulisho hicho cha serikali
hutolewa kwa waandishi walio na sifa za uandishi tu na sio wale waparamia fani
za watu maarufu kama kanjanja.
Ndio! Uandishi
wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine, kwa hiyo kila mwanahabari anatakiwa
kuwa na Press Card ambacho ndicho kitambulisho cha serikali, kama huna basi
wewe sio muandishi au laa hujakomaa kuwa muandishi.
SOMA ZAIDI FATHER KIDEVU BLOG
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...