Na Bashir Yakub
Vijana wengi wajasiriamali wadogo wamefungua makampuni. Hakika wote waliofanya hivi wamefanya jambo jema linaloendana na wakati. Niliwahi kuandika wakati nikielekeza namna nyepesi kabisa ya kufungua kampuni kuwa, ni vigumu kwa leo kufanya biashara na ukawa na mafanikio nje ya kampuni. Nikasema hata kama unauza maziwa, mama ntilie, unauza mayai, kibanda cha huduma ya fedha kupitia simu,unauza mihogo, haizuiwi kufungua kampuni.
Kuna kampuni hata za mtaji wa milioni moja na pesa hiyo si lazima uwe nayo mkononi ila ni katika maandishi tu. Nikasema anayetaka mafanikio kwa sasa ahakikishe hiyo biashara yake ndogo kabisa anaifungulia kampuni.
Kwakuwa wapo wengi ambao tayari wamefungua makampuni basi zipo changamoto nyingi wanazokumbana nazo na kubwa zaidi ni taarifa au ujuzi wa mambo mbalimbali ya namna ya kuendesha kampuni ili kampuni iwe kampuni kweli.
Moja ya eneo lenye shida au ambalo wajasiriamali wadogo hawana taarifa nzuri kuhusu ni taarifa za kodi zinavyolipwa na kampuni kisheria. Hawajui ni kiasi gani, kwa muda gani na vipi. Leo hapa nitaeleza kwa uchache kuhusu kodi za kampuni. Kampuni hulipa kodi ya mapato, swali ni kodi ya mapato nini.
1. KAMPUNI HULIPA KODI YA MAPATO, JE KODI YA MAPATO NINI ?
Kodi ya mapato Tanzania ni tozo kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na vyanzo vitatu ambavyo ni ajira, biashara pamoja na uwekezaji. Aina hii ya kodi inatozwa kwa mamlaka ya Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka 2004, kama ilivyorekebishwa.Kwa upande wetu wa kampuni kodi inayolipwa kwa tafsiri hiyo hapo juu ni kwakuwa kampuni ni biashara na pia ni kwakuwa ndani kampuni waweza kuwamo uwekezaji.Hii ndio sababu kampuni hulipa kodi ya mapato.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Vijana wengi wajasiriamali wadogo wamefungua makampuni. Hakika wote waliofanya hivi wamefanya jambo jema linaloendana na wakati. Niliwahi kuandika wakati nikielekeza namna nyepesi kabisa ya kufungua kampuni kuwa, ni vigumu kwa leo kufanya biashara na ukawa na mafanikio nje ya kampuni. Nikasema hata kama unauza maziwa, mama ntilie, unauza mayai, kibanda cha huduma ya fedha kupitia simu,unauza mihogo, haizuiwi kufungua kampuni.
Kuna kampuni hata za mtaji wa milioni moja na pesa hiyo si lazima uwe nayo mkononi ila ni katika maandishi tu. Nikasema anayetaka mafanikio kwa sasa ahakikishe hiyo biashara yake ndogo kabisa anaifungulia kampuni.
Kwakuwa wapo wengi ambao tayari wamefungua makampuni basi zipo changamoto nyingi wanazokumbana nazo na kubwa zaidi ni taarifa au ujuzi wa mambo mbalimbali ya namna ya kuendesha kampuni ili kampuni iwe kampuni kweli.
Moja ya eneo lenye shida au ambalo wajasiriamali wadogo hawana taarifa nzuri kuhusu ni taarifa za kodi zinavyolipwa na kampuni kisheria. Hawajui ni kiasi gani, kwa muda gani na vipi. Leo hapa nitaeleza kwa uchache kuhusu kodi za kampuni. Kampuni hulipa kodi ya mapato, swali ni kodi ya mapato nini.
1. KAMPUNI HULIPA KODI YA MAPATO, JE KODI YA MAPATO NINI ?
Kodi ya mapato Tanzania ni tozo kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotokana na vyanzo vitatu ambavyo ni ajira, biashara pamoja na uwekezaji. Aina hii ya kodi inatozwa kwa mamlaka ya Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka 2004, kama ilivyorekebishwa.Kwa upande wetu wa kampuni kodi inayolipwa kwa tafsiri hiyo hapo juu ni kwakuwa kampuni ni biashara na pia ni kwakuwa ndani kampuni waweza kuwamo uwekezaji.Hii ndio sababu kampuni hulipa kodi ya mapato.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...