Na   Bashir   Yakub

Vijana wengi  wajasiriamali wadogo wamefungua makampuni. Hakika wote waliofanya  hivi  wamefanya  jambo jema  linaloendana  na  wakati. Niliwahi kuandika wakati  nikielekeza namna nyepesi  kabisa  ya  kufungua kampuni kuwa,  ni  vigumu kwa leo kufanya biashara  na  ukawa  na  mafanikio nje ya  kampuni. Nikasema hata kama unauza maziwa, mama ntilie, unauza mayai, kibanda cha huduma ya fedha kupitia simu,unauza mihogo, haizuiwi kufungua kampuni. 

Kuna kampuni   hata  za mtaji wa milioni moja  na  pesa hiyo si lazima uwe nayo mkononi  ila  ni  katika maandishi   tu. Nikasema anayetaka mafanikio  kwa sasa ahakikishe hiyo biashara yake ndogo kabisa anaifungulia kampuni. 

Kwakuwa wapo wengi ambao tayari  wamefungua  makampuni  basi zipo  changamoto nyingi wanazokumbana  nazo  na kubwa zaidi ni  taarifa au ujuzi wa mambo mbalimbali  ya  namna  ya kuendesha kampuni  ili kampuni  iwe kampuni  kweli. 

Moja ya eneo lenye shida au ambalo  wajasiriamali  wadogo hawana taarifa  nzuri  kuhusu ni taarifa za kodi  zinavyolipwa  na kampuni kisheria. Hawajui  ni kiasi gani, kwa muda gani  na  vipi. Leo hapa nitaeleza kwa  uchache  kuhusu  kodi  za kampuni. Kampuni hulipa  kodi ya mapato,  swali ni  kodi  ya  mapato nini.

1. KAMPUNI  HULIPA  KODI  YA  MAPATO, JE  KODI  YA  MAPATO  NINI ?

Kodi ya mapato Tanzania ni tozo kwa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  inayotokana na vyanzo vitatu ambavyo ni ajira, biashara pamoja na uwekezaji. Aina hii ya kodi inatozwa kwa mamlaka ya Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka 2004, kama ilivyorekebishwa.Kwa upande wetu wa kampuni  kodi inayolipwa kwa tafsiri hiyo hapo juu ni kwakuwa kampuni ni biashara na pia ni kwakuwa ndani kampuni waweza kuwamo uwekezaji.Hii ndio sababu kampuni hulipa kodi ya mapato.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...