Na  Bashir   Yakub
Katika shughuli zetu za kuuza na kununua  ambazo tunazifanya kila siku mikataba ya maandishi  ni jambo ambalo wengi tunakutana nalo. Mikataba hii iwe rasmi au isiwe rasmi suala la msingi ni kuwa  huwa tunaifanya. Aidha wakati mwingine si  wote wenye kuhusisha suala la mikataba ya maandishi  katika makubaliano yaombalimbali  na hii hutokana na  sababu mbalimbali ikiwemo ya kuaminiana. 
Kuhusu kuaminiana niseme jambo moja tu kuwa suala la mikataba ni muhimusana  hata kana  mwenzako unamuamini kwa kiwango cha juu kabisa( highest degree of trust). Nathubutu kusema kuwa hata awe mzazi wako kama kuna jambo la msingi mmelifanya  ni vema kukawapo mkataba wa maandishi.  
Nasema hivi kwakuwa kwa uzoefu wangu wa mambo haya  mara nyingi mgogoro hautokani na waliouziana  au kukubaliana isipokuwa mgogoro unakuja kuanzishwa na walio nyuma ya hao.  Kwa mfano baba anaweza kumpa mwanae kiwanja   na wasifanye  mkataba wowote wa maandishi kwa kuwa wanaaminiana. 
 Hiyo ikaenda kwa miaka kadhaa ambapo baba akawa amefariki. Baaada ya hapo anaibuka mtu anasema mimi  ni mtoto wa  marehemu kwa hiyo nahitaji  kiasi kadhaa kutokamali hii. Hapa mgogoro si kati ya baba na mwana tena   isipokuwa ni kati ya mwana na mtu mwingine. Kama huna mkataba wowote wa maandishi  mpaka kesi hii kuisha waweza kuwa umepoteza kila kitu. 
Huu ni mfano tu katika kusisitiza kuwa mtu asiseme mi na  fulani tunaaminiana. Mgogoro sio lazima utokane na nyie wawili  isipokuwa walio nyuma yenu waweza kuanzisha mgogoro.

MADHARA   YA   KUTOFANYA  MKATABA  WA  KISHERIA .
Ni vema sana kujihadhari kwakuwa ukisikia neno  mgogoro ujue kuna mambo makubwa mawili. 
Kwanza gharama kubwa ni uwezekano wa kupoteza kabisa ilemali na haijalishi iwe uliinunua au ulipewa isipokuwa tu ukishakuwa na mgogoro upo katika hatari hiyo. Pia gharama ya pesa  kama kuwalipa wanasheria, gharama za uendeshaji kesi,  nauli  na matumizi mengineyo ambayo hujitokeza bila hata kutarajia. 
Pili kuna  gharama ya muda . Hii  huhusisha  kushinda mahakamani kila siku  na wote mwajua  mahakama zetu  zilivyo, kushinda vituo vya polisi huku shughuli zako za msingi za kila siku zikisimama. Pia hapa  kuna muda wa  kusubiri hukumu ambapo kesi yaweza kukaa mahakamani hata miaka  sita . Hakika unakuwa umesurubika(suffer) na  umepoteza mambo mengi katika kushughulikia jambo hili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...