Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii wa Jamuhuri ya muungano Mhe.Bw.Seif Rashid na waziri wa afya wa ZanzibarMhe. Rashid Seif Suleiman, Siku
ya jumapili 25 januari 2015 walikutana na kuongea na baadhi ya
watanzania waishio nchini ujerumani katika hoteli ya Martim Hotel mjini
Berlin.
Mawaziri hao kwa pamoja waliongozana na balozi Tanzania nchini
Ujerumani mheshimiwa Bw.Philip Malmo,katika mkutano huo mawaziri hao
wote walielezea jinsi wizara zao zinavyofanya kazi kuhakikisha kuwa
huduma za afya zinawafakia walio wengi na pia kuhakikisha siku za usoni
kila Mtanzania atatanufaika na huduma hizo kwa kutumia bima ya afya bila
kujali tofouti za uwezo wa vipato vyao.
Watanzania waishio ujerumani
wamefarajika sana na mkutano huo,pia mawaziri wamewataka watanzania
waishio ughaibuni kuchangia kuwekezakatika
sekta ya huduma ya afya hata ikiwa ni sekta binafsi ,mawaziri hao
wamesema milango ya wizara zao hipo wazi kwa watanzania wanaotaka
ushauri,ushirikiano au kuwekeza katika sekta hizo.
Kamanda
Ras Makunja wa Ngoma Africa(katikati)makam mwenyekiti wa UTU Bw.Peter
Kazaura(mwenye kitamba shingoni) mdau Shah wa jiji la Berlin Mwenye
kofia nao walikuwapoMkuu wa bendi ya Ngoma Africa Kamanda Ras Makunja akiwa Mhe.Philip Malmo Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ,katika mkutano katika hoteli ya Maritim mjini Berlin.
Waziri wa Afya na ustawi wa jamii ambaye pia ni mbunge wa Rufiji Mhe.Seif Rashidi akiwa na Ebrahim Makunja aka Ras Makunja mjini Berlin,Ujerumani. Waziri wa Afya wa jamuhuri ya muungano mhe.Seif Rashidi akiongea na watanzania waishio Ujerumani,
Waziri wa Afya wa Tanzania Mhe.Seif Rashid akiwa na baadhi ya watanzania nchini Ujerumani.
Naona waziri yupo na watanzania wa ujerumani harafu kamanda Ras Makunja naona kajikoki kila kitu ukimchokoza tu virungu
ReplyDeleteeh! bwana saralehh kamanda ras makunja umependeza uko Berlin naona upo uraiani kama raia wengine
ReplyDeletehaya bi jokha na sele na waona full kujiachia, mjomba shah kumbe ulikuwepo nice, haya twambieni mlikuwa na hoja gani na mmekubaliana nn? maana mh amemuondoa mh Mwakyembe sehemu ambayo alikuwa anaiweza na anawaweza leo hii sijuwi kapelekwa wapi? mliileta hiyo hoja?
ReplyDeletekamanda ras makunja akiwa katika vazi kiraia nje ya jukwaa katulia tena binadamu kweli kweli
ReplyDeleteweh Peter Kazaura huyo mliyemweka katu chui wa nguvu ukivuka anga zake anakujerui
ReplyDeleteRas Makunja hiyo pete yako nikuvue nimefika bei
ReplyDeletete !te! Kikamanda ketu ras makunja kilikuwepo kimependeza kweli uraiani
ReplyDeletenaona kamanda ras makunja umejinyonga si mchezo umependeza,una haja tena ya kuvaa gwanda
ReplyDeletewewe ras makunja utaki kupiga konozz? kwa wadada au ndio umeuchuna unajifanya kipofu
ReplyDelete