Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein (wa tatu kulia) Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Amani Abeid
Karume (kulia) na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Balozi Seif
Ali Iddi pamoja na Viongozi wengine na waislamu mbali mbali wakijumuika
kwa pamoja kumswalia aliyekuwa Mshauri wa Rais wa Utalii Marehemu Issa
Ahmed Othman katika Masjid Mahfoudh Mazizini, Marehemu alifariki juzi
Nchini India na kuzikwa leo Kianga Wilaya ya Magharibi Unguja.
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein, (katikati)Rais Mstaafu wa Zanzibar Alhaj Dk.Amani Abeid Karume,
Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Balozi Seif Ali Iddi pamoja na
Viongozi mbali mbali na Waislamu mbali mbali wakijumuika kwa pamoja
kumuombea dua baada ya kumswalia aliyekuwa Mshauri wa Rais wa Utalii
Marehemu Issa Ahmed Othman katika Msikiti Masjid Mahfoudh
Mazizini,Marehemu amezikwa leo Kijiji cha Kianga Wilaya ya Magharibi
Unguja,


Baadhi
ya Vijana na wananchi waliobeba Jeneza la Marehemu Issa Ahmed Othman
aliyekuwa Mashauri wa Rais Utalii Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
wakiupeleka kuzikwa kijijini Kianga Wilaya ya magharibi Unguja leo
jioni,marehemu alifariki juzi Nchini India ambako alikwenda kwa
matibabu,[Picha na Ikulu.]

Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed
Shein na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhaj Balozi Seif Ali Iddi
(katikati) pamoja na Viongozi wengine na waislamu mbali mbali
wakijumuika kwa pamoja katika mazishi ya aliyekuwa Mshauri wa Rais wa
Utalii Marehemu Issa Ahmed Othman katika Kijiji cha Kianga Wilaya ya
Magharibi Unguja leo jioni,[Picha na Ikulu.]
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...