Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb) ameondoka nchini tarehe 13 Januari 2015 kwenda Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Mhe. Sergey Lavrov.
Ziara hiyo inalenga kuimarisha na kupanua ushirikiano kati ya Tanzania na Urusi.
Mhe. Membe anatarajiwa kutumiafursa hiyo kuhimiza ushirikiano wa kiuchumi na Urusi, hususan katika maeneo ya biashara, uwekezaji na ubadilishanaji wa teknolojia. Tanzania inaweza kufaidika na utaalamu wa Urusi katika sekta za uzalishaji wa nishati, uvuvi, afya, kilimo na huduma.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Tarehe 14 Januari, 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...