1
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Damian Lubuva akizunguza na waandishi wa habari kwenye makao makuu ya tume ya uchaguzi jijini Dar es salaam wakati alipozungumzia maandalizi ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura, kura ya maoni ya Katiba mpya na uchaguzi mkuu mwezi oktoba mwaka huu, kulia ni Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Bw. Julius Mh.Julius Mallaba.
2
Baadhi ya waadishi wa habari wakiwa katika kutano huo.


NA CHALILA KIBUDA ,GLOBU YA JAMII DAR

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inatarajia kutumia Bilioni 293 kwa ajili ya uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura kwa mwaka huu ikiwa ni lengo kukuza demokrasia nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo ,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema wamejipanga kuhakisha watu wenye sifa za kupiga kura wanajiandikisha ili waweze kupiga kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa  pamoja na kupiga kura ya uchaguzi mkuu   Oktoba mwaka huu.

Lubuva alisema kuwa suala la kuwepo wanajeshi katika uchaguzi , wataangalia jinsi gani  ya kufanya  na kazi ya ulinzi ibaki mikononi  mwa jeshi la polisi.

‘’Suala la ulinzi wa jeshi  tuliweke na kuangalia jinsi gani tutafanya katika kuhakikisha wananchi wanapiga kura kwa amani na usalama wa mali bila kuwa na hofu ya watu wanaowalinda’’alisema  Jaji Mstaafu Damian Lubuva.

Aidha alisema uandikishaji wa majaribio, utambuzi wa alama ya mpiga kura kwa kifaa cha BVR ulikwenda vizuri na mapungufu yaliyojitokeza wataendelea kuboresha ili kila mtanzania aweze kujiandikisha na kupiga kura.

Alisema uandikishaji wa kanda ya kwanza utaanza Februari 16 hadi Machi 15 ambapo hakutaja mikoa gani itaanza hivyo wanaandaa orodha ya mikoa na kanda katika jinsi ambavyo daftari la kudumu la mpiga  litavyoweza kupita  kuandikisha.

‘’Mambo yote yatakwenda sawa baada kukamilika kwa daftari la mpiga kura likiwemo upigaji kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa  na maoni ya wadau yataendelea kupokelewa katika ofisi yetu’’alisema Jaji Lubuva 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Tunaomba na sisi tulio nje ya nchi turuhusiwe kujiandikisha kupitia Balozi za nchi yetu.Hoja hii inaenda samba samba na jinsi tulivyoona wakati wa kupiga kura kwa wajumbe wa Bunge la katiba waliokuwa nje ya nchi.

    ReplyDelete
  2. Hoja yako tutaifanyia kazi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...