Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(katikati)akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa uzinduzi wa Promosheni mpya inayojulikana kama JayMillions itakayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kujishindia zawadi mbalimbali zenye thamani ya Shilingi Bilioni 30/- Ili kujua kama umeshinda mteja anatakiwa kutuma SMS moja tu yenye neno “JAY” kwenda namba 15544 kila siku.Kushoto ni Balozi wa promosheni hiyo Hilary Daud”Zembwela” na kulia ni Meneja Uhusiano wa Umma wa kampuni hiyo Matina Nkurlu.
Balozi wa promosheni ya JayMilions Hilary Daud ”Zembwela” (kushoto) akionesha bango linaloelezea jinsi ya mteja kujua kama ameshinda katika Promosheni hiyo iliyozinduliwa na Vodacom Tanzania leo itakayowawezesha wateja wa kampuni hiyo kujishindia zawadi mbalimbali zenye thamani ya Shilingi Bilioni 30/- Ili kujua kama umeshinda mteja anatakiwa kutuma SMS moja tu kila siku yenye neno “JAY” kwenda namba 15544.Wengine kutoka kulia Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu na Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo Kelvin Twissa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...