Na Chalila Kibuda na Globu ya Jamii 

Imeelezwa kuwa watahiniwa 2,175 sawa na asilimia 46.9 wameshindwa kufaulu mitihani ya Bodi ya Uhasibu na Ukaguzi (NBAA).

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA,Pius Maneno ilisema kuwa mitihani hiyo ya kwanza katika mfumo mpya  wa elimu wa mafunzo unaozingatia weledi na matokeo hayo hayalinganishwi  na matokeo ya nyuma ilifanyika katika mfumo wa kukazia maarifa.

Kwa mujinu wa Maneno,watahiniwa waliojisajili ni 6,464  kati ya hao 678 sawa na asilimia 10.5 hawakuweza kufanya mtihani kwa sababu mbalimbali.

Taarifa hiyo imesema watahiniwa 1,260 wamefaulu mtihani ngazi husika ,watahiniwa 1,811  wamefaulu baadhi ya masomo  katika ngazi ngzi husika.

Jumla ya watahiniwa 356  ikiwa wanawake 95  na wanaume 261 wamefaulu mtihani wa shahada ya juu ya uhasibu nchini (CPA)  na kufikia watalaam  wa CPA 6002 tangu ianze mitihani hiyo mwaka 1975.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...