Vijana na wazee wa kiIslamu wa MwembeTanga wamefanikisha kuadhimisha Maulid ya Mtume Muhammad Salallahu alayhi wasalam, yaliosomwa Siku ya Jumanne Jan 13 ,2015 sawa na Rabii Awal 1436
Maulidi hayo walioaza rami mida ya Saa tatu usiku maraa tu baada kusaliwa sala ya Ishaa, katika Mtaa wa Mwembetanga maarufu (Kwa Karagosi) Zanzibar ambapo Wazee na vijana hao huuandaa maulidi kila mwaka, ifikapo mwezi wa kuzaliwa Mtume Muhammed S.A.W.

Muongozaji Maulidi ya Mwembetanga kwa karagosi MC Imam Sadat Fadhil Abdullah akiongea Mipangilio ya maulid kwa ratiba maalumu iliopangwa na wana kamati Ya maandalizi ya Maulidi hayo.

Wazee wa mtaa wa M/Tanga Hajji AbdulAziz akiea na Sheik Ahmed wakiwa makini kusikiliza maulid ya Mtume Muhammad Salallahu alayhi wasalam, yalioandaliwa na vijana pamoja na wazee wawa MwembeTanga Siku ya Jumatatu Jan 13, 2014 Zanzibar.

Waumini wa kiIslamu kutoka maeneo mbali mbali wakiwa katika maulid ya Mtume Muhammad Salallahu alayhi wasalam, yalioandaliwa na vijana pamoja na wazee wawa MwembeTanga Siku ya Jumatatu Jan 13, 2014 Zanzibar.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...