Kama ilivyo kawaida ya watu wa maeneo mengi hapa nchini,kwamba likitokea la kutoka basi huwa ni faida kwa watu wengine.Mchana wa leo katika Makutano ya barabara ya Nyerere rodi na Kawawa rodi,gari ndogo aina ya Toyota Hilux iliyokuwa imebeba Vioo ilipatwa na mkasa na kupelekea mzigo wa vioo hivyo kuanguka katikati ya barabara na kupasuka,hali iliyowapelekea vijana wanaofanya biashara za mikononi (maarufu wa machinga) katika eneo hilo kuingia barabarani na kuanza kujibebea mabaki ya vioo hivyo kama ionekanavyo pichani hapa.hali iliyopelekea magari mengine yaliyokuwa yakiitumia njia hiyo kuwakwepa vijana hao ili waendelee na kazi yao ya kujisevia vioo. 

Hali hiyo ilidumu kwa muda kidogo na kupelekea Askari wa usalama barabarani kuyaongoza magari kupita pembezoni mwa barabara hiyo ili kuwaacha vijana hao ambao hawakutana kusikia la muadhini wala la mnadi swala.
 Kazi ikiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. yote hiyo ni njaa tu. Basi hiyo ndo Tanzania yetu, watu wote hawawezi kua na ajira sawa. Wengine ndo wanajiajiri kama hivyo waonekanavyo. Kila jema wapendwa

    ReplyDelete
  2. hata kama vijana hao wasingekuepo bado magari yangeongozwa hivyo hivyo. tena itakuwa wamesaidia madereva wasiingie kukanyaga vioo hivyo

    ReplyDelete
  3. Yote hii ni "NZALA"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...