Mkuu wa Biashara za Kimtandao wa Copy Cat Tanzania Limited,Jonnavithola Prasad akizungumza na waandishi wa habari juu uzinduzi wa kifaa cha kuzuia wizi wa mtandao na jinsi walivyojipanga katika kutoa ushauri wa kifaa hicho katika hafla  hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam jana.
Mshauri wa Teknolojia na Biashara wa Copy Cate Tanzania Limited, Nathalie Ayonga akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya uzinduzi wa kifaa cha kuzuia wizi wa mtandao, hafla hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam jana.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Kampuni ya Copy Cate Tanzania Limited wamezindua mfumo wa kuzuia wizi katika mtandao ambao una uwezo mkubwa wa kuzuia kwa mtu mmoja mmoja au kundi lililo katika mtandao mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari jana  katika ukumbi wa  Hoteli Hyatt Regency,Jijini Dar es Salaam,Mshauri wa Masuala ya Teknolojia ,Biashara,Naththalie Ayonga ,alisema  mfumo huo katika mitandao utasaidia taasisi za serikali  sekta binafsi  na mtu mmoja moja kuweza kudhibiti  wizi wa taarifa katika mitandao.

Ayonga alisema kampuni imekuwa ikifanya kazi za mafanikio katika mfumo wa mabadiliko wa teknolojia kwa kuweza kufanya ingiaji wakati uzinduzi wa kimfumo katika karne ya 21 ya sayansi na Teknolojia.

Alisema kifaa hicho cha kuzuia wizi wa taarifa katika mitandao  wa mfumo huo kimekuja kwa wakati mwafaka kwa Tanzania kutokana na kuwepo watu wengi kuingia katika teknolojia za mitandao bila kuwa na ulinzi.

Kifaa cha mfumo kinajulikana kama Cisco ambacho kimekuwa na chachu kudhibiti wizi katika mitandao hivyo ni fursa ya watazania kupokea katika kulinda taarifa zao zisiingiliwe na mtu mwingine.


Kampuni ya Copy Cat Tanzania Limited  ndio itakuwa inafanya masuala ya kifumo katika mitandao na uingizaji wa bidhaa mpya  na ambayo ilikuwa ikifanyw na BMTL.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...