Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Dkt. John Pombe Magufuli amelaani vikali tukio la kikatili la kutekwa na kuuawa kwa mtoto Yohana Bahati pamoja na kujeruhiwa vibaya kwa mama mzazi wa marehemu na watu wasiofahamika.

Akizungumza kwa masikitiko makubwa jijini Dar es Salaam, Dkt.Magufuli amewataka Watanzania kuishi kwa amani na upendo na kuacha dhana ya kutajirika kutokana na viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi(Albino).

“Tukio hili ni la kinyama na halikubaliki popote Duniani, watu wanatakiwa waelewe kuwa mtu huwezi kutajirika kutokana na viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi kama alivyofanyiwa mtoto Bahati” Alisema Waziri Magufuli.

Katika hatua nyingine, Waziri Magufuli ametoa msaada wake wa awali kiasi cha Shilingi milioni Moja kwa ajilili ya kumsaidia Ester Jonas mama mzazi wa mtoto huyo aliyeuawa na watu hao wasiofahamika.

“Nimeona nitoe msaada wangu wa awali kiasi hichi cha fedha kwa ajili ya kumsaidia mama huyu aliyejeruhiwa vibaya kwa ajili ya mahitaji yake mbalimbali na hapo badae ntakapopata nafasi ntakwenda nyumbani kwake kutoa pole zaidi”

Aidha, Waziri Magufuli ameishukuru Hospitali ya Wilaya ya Chato pamoja na Bugando kwa msaada mkubwa wa kumpatia matibabu mama huyo aliyejeruhiwa vibaya na watu hao wasiofahamika.

Pia Waziri Magufuli aliipongeza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita kwa kazi kubwa ya kuwatafuta wale wote waliohusika na tukio hilo la kikatili.
Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato mkoani Geita Dkt. John Pombe Magufuli(kushoto) akikabidhi msaada wa fedha Shilingi Milioni Moja kwa Mwandishi wa ITV Ndugu Emanuel Buhohela(kulia) kama mchango wake wa awali kwa ajili ya kumsaidia Ester Jonas aliyejeruhiwa vibaya na watu wasiofahamika wakati wa tukio la kutekwa kwa mwanaye mwenye ulemavu wa ngozi(Albino) Yohana Bahati aliyeuwawa katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita. Mama huyo bado amelazwa katika katika Hospitali ya Bugando kwa ajili ya matibabu. Habari na Picha kwa Hisani ya Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ma engineer. Wa jiji acheni kukaa ofisini na fanyeni kazi sio mnakaa tu ujenzi karibu wote. Unayofanyika sasa na makarandasi iko chini ya kiwango mnagojea mpaka Ajali itufikiye. Mheshimiwa slaa watu wako. Hawafanyi kazi zao fanya mabadiliko

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...