Mfuko wa Pensheni wa GEPF umesaini mkataba wa uwekezaji na Bodi
ya Wahasibu na Wakaguzi (NBAA) katika eneo la Bunju. Uwekezaji huo
utakaohusisha kumbi za mikutano (Conference Halls) zenye uwezo wa
kuchukua watu Zaidi ya 1,200, migahawa (Restaurants), Hoteli yenye
hadhi ya kimataifa yenye vyumba Zaidi ya 102, Maktaba, Bwawa la
kuogelea (Swimming Pool) pamoja na sehemu za mazoezi (Gymnasium)
Uwekezaji huo utagharimu Zaidi ya shilingi Bilioni 33 za kitanzania na
unategemewa kukamilika katikati ya mwaka huu 2015.
Mkurugenzi Mkuu wa GEPF, Daud Msangi (wa pili kulia) akiongoza majadiliano
ya awali kati ya Menejimenti ya GEPF pamoja na Menejimenti ya NBAA
kabla ya zoezi la kutiliana saini mkataba wa uwekezaji.
Mwenyekiti wa Bodi ya GEPF,Bi. Joyce Shaidi (kulia) pamoja na mwenyekiti
wa NBAA Profesa Issaya Jairo wakisaini mkataba wa ushirikiano wa
uwekezaji wa pamoja wakiongozwa na mwanasheria wa NBAA Bi
Agness Kessy.
Utiaji saini huo ulishuhudiwa na makamu mwenyekiti wa NBAA Bi
Anna Mbughuni ( mwenye suti ya blue), Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA
Bw Pius Maneno, Mkurugenzi Mkuu wa GEPF Bw Daud Msangi pamoja
na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GEPF Bw Festo Fute.
Mwenyekiti wa Bodi ya GEPF Bi Joyce Shaidi akibadilishana nyaraka
za mkataba wa uwekezaji wa pamoja na Mwenyekiti wa NBAA Profesa
Issaya Jairo.
Pichani baadhi ya watendaji wa Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi
(NBAA) wakifurahia jambo mara baada ya zoezi hilo kukamilika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...