Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Chande Othman akiongozana na Mhe. Robert Makaramba alipopokelewa mapema leo katika Uwanja wa Ndege Mwanza, nyuma ni baadhi ya Maafisa wa Mahakama wa Mkoani Mwanza waliofika kumpokea Mhe. Jaji Mkuu.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania (kushoto). akifurahia jambo na Mhe. Jaji Robert Makaramba, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, katika chumba maalum cha wageni (VIP room) alipofika mkoani Mwanza mapema leo tayari kwa ziara ya Kutembelea Mahakama mkoani Tabora atakayoanza rasmi kesho.
Mhe. Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akisaini kitabu cha wageni ktk chumba maalum cha wageni (VIP) katika Uwanja wa Ndege jijini Mwanza. (Picha na Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania).
Mhe. Mohamed
Chande Othman, Jaji Mkuu wa Tanzania, akisalimiana na mmoja wa Maafisa wa
Polisi Mkoani Mwanza alipowasili katika Uwanja wa Ndege Mwanza mapema leo kwa
ajili ya safari ya kuelekea mkoani Tabora kwenye ya KIKAZI,ikiwa ni pamoja na
kukagua utendaji kazi wa Mahakama mkoani humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...