Wakopwaji/wadaiwa  wamekuwa  wakipata shida sana  kutoka  kwa wanaokopesha. 
Mkopesha awe ni mtu binafsi, taasisi ya fedha , kampuni  binafsi au mwingine  yeyote  wamekuwa  wakiwasumbua sana  wadeni  wao. 
Kubwa  zaidi hasa taasisi za fedha hutumia masharti ya mikataba ambayo  huwa yameandaliwa kitaalam kiasi cha  mtu ambaye  si mwanasheria  kutoelewa kwa undani maana  yake  kuwabana wadeni  ambao  hushtukia  masharti hayo baada  ya  kuwa wameshaanza  kudaiwa. 
Mbaya  zaidi  wamekuwa  wakifanya hivi bila kufuata taratibu za kisheria. Kwakuwa wamemsaidia  mtu kwa kumkopa   basi  wamekuwa  wakiichukulia  hali  hiyo kama  leseni ya  kufanya  lolote  ilimradi  tu  wanadeni  na wewe. 
Mali  za watu  huuzwa  hovyo  , wengine hufikishwa  mpaka   vituo  vya polisi  ilimradi  tu wakopeshaji   hupenda  kupindisha  utaratibu. Hapa  tutaeleza  baadhi  ya  mambo  kadhaa  ya msingi  ambayo  mkopeshaji  haruhusiwi kumfanyia  mdeni. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...