HOSPITALI ya Kumbukumbu ya Kairuki Mikocheni jijini Dar es Salaam, imeingiza mtambo maalumu wa kisasa kutoka Kampuni ya Ethicon ya Marekani utakaokuwa ukitumika katika upasuaji wa kawaida na ule matobo.
Mtambo
huu unafahamika kama Ultrasonic and Advanced Bipolar
HARMONIC Generator unatumia nishati ya sauti au mwangwi (ultrasound) kuweza kukata mwili wa binadamu bila kupoteza hata chembe ya damu kwa mgonjwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Daktari Bingwa wa Upasuaji katika hospitali hiyo, Dk. Muganyizi Kairuki alisema kuwa mtambo huo unaweza kupunguza athari zinazoweza kutokea kwa viungo vya jirani wakati wa upasuaji kama ilivyo kwa mitambo ya zamani inayotumika sasa katika hospitali nyingine.
Dk. Muganyizi aliongeza kuwa faida za mtambo huo ni
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Daktari Bingwa wa Upasuaji katika hospitali hiyo, Dk. Muganyizi Kairuki alisema kuwa mtambo huo unaweza kupunguza athari zinazoweza kutokea kwa viungo vya jirani wakati wa upasuaji kama ilivyo kwa mitambo ya zamani inayotumika sasa katika hospitali nyingine.
Dk. Muganyizi aliongeza kuwa faida za mtambo huo ni
kurahisisha na kuharakisha upasuaji hivyo kupunguza muda wa upasuaji kwa jumla na kuondoa kabisa matumizi ya nyuzi za kushonea viungo vya ndani wakati wa upasuaji.
"Mtambo huo unapunguza matumizi na mahitaji ya damu ambayo ni adimu kupatikana kwa wagonjwa wanaofanyiwa upasuaji hospitalini". alisema Dk. Muganyizi.
Mtambo maalumu wa kisasa kutoka Kampuni ya Ethicon
ya Marekani utakaokuwa ukitumika katika upasuaji wa kawaida na ule
wa matobo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...