Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam imezuia maandamano ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya Ilala (UVCCM) ya kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa chama hicho pamoja na kuacha kiporo  maandamano ya Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bawacha).

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam ,Kamishina wa Jeshi la Polisi ,Suleiman Kova ,amesema kuzuia kwa maandamano hayo inatokana na kuwepo kwa taarifa za Kiintelejensia za kuvuruga amani.

Kova amesema maandamano ya UVCCM Wilaya ya Ilala yalitakiwa kufanyika kesho lakini kutokana na kuwepo kwa taarifa za kiintelejensia za Machinga ,Bodaboda ,Mama Lishe na Baba Lishe kushiriki maandamano na kufikisha malalamiko yao kupitia maandamano hayo.

Amesema kumekuwepo kwa taarifa katika mitandao ya jamii wakihamasishana bodaboda na machinga ,mama lishe na baba lishe kushiriki maandamano pamoja na kutoa ujumbe wao kwa kupitia maandamano katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Kova amesema machinga ,Mama lishe,Baba,na Bodaboda watumie taratibu zingine za  kufikisha ujumbe kutokana na sheria zilizowekwa na sio kutumia mgongo katika vyama vya siasa.

Kwa upande  Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) maandamano yao yalikuwa yanahusu kwenda tume ya Taifa ya Uchaguzi ni lini itaanza kuandikisha daftari la wapiga kura ,pamoja na wanafunzi watashiriki vipi upigaji kura ambapo Kamanda Kova amesema hilo wanaweka kiporo kwanza wanafanya uchunguzi wa taarifa mbalimbali.

“Sisi tunachoangalia amani kwani maandamano ya amani yanaweza kufanyika lakini mwisho wa siku inakuwa sio amani kwa jeshi la polisi tunawajibu kuangalia hilo”amesema Kamanda Kova.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...