Mkurugenzi wa Kampuni ya Ibraline ,Ibrahim Shayo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Moshi.



SIKU chache baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kutangaza punguzo la bei ya Mafuta Kampuni ya kutoa huduma ya usafirishaji wa ndani na nje ya nchi ya Ibraline imetangaza kushusha nauli kwa nusu ya bei elekezi ya SUMATRA.

Hatua hiyo inakuja wakati baadhi ya wananchi kulalamika kutokuwepo na ahueni yoyote licha ya kwamba serikali imetangaza kushusha bei ya bidhaa ya Mafuta kwa nchi nzima kufuatia  bidhaa hiyo kushuka bei katika soko la dunia.

Akizungumza ofisini kwake mkurugenzi wa Kampuni hiyo Ibrahimu Shayo alisema Kampuni imefikia hatua hiyo ikiwa ni sehemu ya kutoa shukurani kwa wateja wake ambao wamekuwa wakitumia huduma ya usafiri inayotolewa na Ibraline.

“Tumeamua kufanya hivi lengo ni kuwashukuru wateja wetu wanao tumia huduma ya usafiri unaotolewa na kampuni yetu ya Ibraline…ningewajua mmoja mmoja ningeweza kuwapa mkono lakini kwa kuwa wanaishi maeneo tofauti ndio sababu tumeamua kurudisha kile tunachopata kwa njia ya kuwapunguzia bei.”alisema Shayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...