Wala hakosei kusema ‘kujua kazi ni raha’. Isha Mashauzi anakushuka tena kivingine na wimbo mpya kabisa “Nimpe Nani” unaodhihirisha kuwa anaijua vema kazi yake.
Hii ni ‘single’ yake ya pili nje ya taarab ukiacha ule wa kwanza “Nimlaumu Nani” uliopigwa katika miondoko ya rhumba.
“Nimpe Nani” ni wimbo unaoelea kwenye miondoko ya zouk rhumba lakini ukikolezwa kwa mbali na vionjo vya mduara.
Wimbo huo wa dakika tatu na nusu ambao umerekodiwa katika studio za C9 Records chini ya producer C9 Kanjenje.
Kinanda kimepigwa na Kali Kitimoto na C9, magitaa ya bass na solo yamepigwa na Babu Bomba wa Malaika Band.
Sauti zote tamu unazozisikia humo ni za Isha Mashauzi kasoro sehemu ndogo sana isiyozidi sekunde 5 iliyotikiwa na Easy Man.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...