Na   Bashir     Yakub.

Mara nyingi  nimeandika  kuhusu  mirathi  lakini  zaidi  nimegusia habari ya usimamizi  wa mirathi . Leo  nimeona  ni muhimu  kueleza  mgao  wa mirahi  kwa kuangalia nani anapata  nini kupitia  Sheria ya mirathi ya serikali. Fuatana  nami.

( A ) MGAO UKOJE  IKIWA  MUME  AMEFARIKI  AKAACHA  MJANE, WATOTO  NA  NDUGU ZAKE.

Kama mume  amefariki  na akaacha mjane na watoto basi moja ya tatu ( 1/3) ya mali  za marehemu  zilizo kwenye mirathi anatakiwa apewe mke wake. Mbili ya tatu( 2/3)  ya mali hizo itaenda kwa watoto wake.

( B ) MGAO UKOJE KAMA MAREHEMU HAKUACHA WATOTO  LAKINI   KUNA  MJANE.
Kama hakuna watoto walioachwa  na marehemu katika familia husika  lakini kuna mjane ,mali ya marehemu hugawanywa katika mtindo ambao ndugu hupewa nusu (1/2), na mjane  hupewa nusu ya mirathi ya marehemu(1/2). Hii ni sawa kwa sawa.

(C)MGAO UKOJE IWAPO MAREHEMU HAJAACHA NDUGU WALA   MTOTO ISIPOKUWA MJANE TU.

Kama marehemu hajaacha ndugu wala  mtoto  au watoto  basi mali yote huchukuliwa  na  mjane.Ndugu  kwa maana  ya hapa ni  kaka, dada, mama  mzazi  wa marehemu au baba n.k. 
( D ) KAMA  MKE AMEFARIKI  NA KAMUACHA  MUME  NA  WATOTO JE   MGAO  UKOJE.

Hapo juu tumeona mume akifariki akamuacha mke  na watoto mke huchukua  moja ya tatu na watoto au mtoto mbili ya tatu. Hali  iko hivohivo kwa mume naye ana haki kama alizo nazo mke wake yaani kupata mirathi kutoka katika mali za marehemu.Kwa maana hiyo mume hupata moja ya tatu(1/3)  ya  mali  za marehemu mkewe na mbili ya tatu (2/3) huenda kwa watoto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...