Baada ya kikao kilichofanyika wiki iliyopita chuo
kikuu cha Stafford ambapo Rais Obama wa marekani alikutana na wafanya biashara,
Wanasheria na wasimamizi washeria kujadili hali ya mtikisiko wa maswala ya
usalama mitandao, Inadhihirisha wazi bado kuna safari ndefu kukabiliana na
wimbi hili la uhalifu mtandao duniani kote.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba Tishio la uhalifu
mtandao na utayari wa kukabiliana nao bado kuna kutowiana ipasavyo ingawa
jitihada bado ni kubwa kuweza kukabiliana na uhalifu huu unaokua kwa kasi ya
pekee duniani kote.
Nategemewa kuwasilisha mada itakayoangazia jitihada za
mataifa makubwa 8 dhidi ya uhalifu mtandao na athari za jitihada hizo kwa
mataifa mengine katika mkutano wa mwaka utakaofanyika Nchini Croatia
unaounganisha wataalam wa maswala ya usalama mitandao kutoka mataifa kadhaa
ambapo patajadiliwa mambo kadhaa ya kiusalama mitandao – Taarifa Zaidi za
mkutano zinaweza kupatikana kwa "KUBOFYA HAPA"
Wakati haya yakijiri na mikakati Zaidi ikiendelea ya
kukabiliana na wimbi kubwa la uhalifu mtandao hivi sasa makampuni
yanayojihusisha maswala ya fedha yameonekana yakiathirika Zaidi na uhalifu
mtandao – Hii ni kwamujibu ya ripoti maalum iliyotolewa na kampuni ya Kaspersky
Lab.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...