Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (katikati) akiwa katika kikao kilichojumuisha watendaji wa TANESCO, REA, na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika mikoa ya Lindi na Mtwara. Kulia kwa Waziri ni, Mhandisi Nishati Mwandamizi, kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Salum Inegeja na kushoto ni Mhandisi Thomas Visi, Meneja wa kampuni ya Naomis Corporate Ltd inayotekeleza miradi ya usambazaji umeme vijijini katika mkoa wa Mtwara.
Mhandisi Mkuu Usambazaji Umeme katika mikoa ya Dar es Salaam, Benedict Lyaruu (wa kwanza kulia), Kaimu Meneja wa TANESCO, mkoa wa Pwani, Eng. Rehema Mashinji (katikati) na Mhandisi Miradi ya Umeme katika mkoa wa Pwani, Leo Mwakatobe (kushoto) wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage (haonekani pichani) wakati wa kikao chake na watendaji wa TANESCO, REA, na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika miko ya Lindi na Mtwara.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...