BONDIA Fransic Miyeyusho 'Chichi Mawe' 


ametamba kumsambalatisha Fadhili Majiha 'Stopper' katika raundi za awali za mpambano wao utakaofanyika siku ya jumamosi ya feb 28 katika uwanja wa ndani wa taifa mpambano huo wa raundi nane unasubiliwa kwa hamu kubwa na mashabiki mbalimbali wa mchezo wa masumbwi nchini ususani vitongoji vya Kinondoni, Manzese, mabibo na Mwananyamala ambapo ndio maeneo yao yenye wapenzi wao wa ngumi na sehermu mbalimbali


akizungumza na mwandishi wa habari hizi Miyeyusho ametamba kuwa atokuwa na mzaha siku hiyo itakuwa kazikazi mana yeye ni bondia mkubwa sana hapa nchini na akuna mtu wa kumbabaisha kwa sasa katika uzito wake

mbali na mpambono huo wa utangulizi kutakuwa na mpambano wa ubingwa wa U.B.O Africa utakaowakutaniosha mabondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' na Cosmas Cheka kutoka Morogoro ambao watatanguliwa na mapambano mengine yatakayowakutanisha Shomari Mirundi zidi ya Mwinyi Mzengela wakati Shedrack Ignas atapambana na Husein Mbonde, na Godfrey Slive atamenyana na Sadick Abdulazizi


siku hiyo kutakuwa na uzwaji wa DVD za ngumi  mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywether, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis, David Haye,Mohamed Alina wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...