Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya EY, Bw. Mark Otty, amesema Tanzania ina rasilimali nyingi ambazo zinahitaji watu kuwekeza, hasa katika sekta ya miundombinu, kilimo, huduma za Kifedha ,mawasiliano,madini pamoja na gesi asilia .
Otty ameyasema hayo leo wakati wa alipokutana na waandishi wa habari kwenye ofisi ya kampuni hiyo hapa nchini,yenye makao yake makuu nchini Uingereza,amesema kutokana na rasilimali zilizopo zitavuta uwekezaji na uchumi wa nchi unaweza kukua.
Mkurugenzi huyo amesema kazi kubwa ya kampuni hiyo ni ushauri wa uchumi ,biashara pamoja na ukaguzi kwa sekta za serikali na sekata binafsi.
Amesema katika ziara yake nchini ni pamoja na kukutana na Rais Jakaya Kikwete na kujadili masuala mbalimbali likiwemo la ujio wake nchini na jinsi kampuni yake na serikali wanavyoshirikiana katika shughuli mbalimbali za biashara.
Kwa upande wa Meneja Mkazi wa Kampuni ya EY, Bw. Joseph Sheffu amesema kuna maeneo mengi wameayatafiti na kuona kuna fursa ya uwekezaji kutokana na taratibu bora zilizopo nchini katika sekta ya uwekezaji.
Bw. Sheffu amesema kampuni hiyo ina wahasibu,wataalam wa kodi pamoja na wakaguzi ambao wameweza kupata ujunzi katika mataifa mbalimbali  hivyo huduma inayotolewa na taasisi hiyo imekuwa ni bora.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya EY,Mark Otty akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) alipokutana nao Februari 24,2015 kwenye ofisi za kampuni hiyo,jijini Dar es salaam.
Meneja Mkazi wa Kampuni ya EY, Bw. Joseph Sheffu (kushoto) akifafanua jambo kwa wanahabari (hawapo pichani) wakati walipokutana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya EY, Bw. Mark Otty (kulia) kuzungumzia ujio wake hapa nchini. Picha na Othman Michuzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...