Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro akiongea na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora jijini Dar es Salaam jana (Jumanne, Feb 24, 2015). Kulia kwake ni Naibu Waziri Ummy Mwalimu na kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Tume hiyo Wakili Bahame Tom Nyanduga na Katibu Mtendaji Bi. Mary Massay. Waziri alifanya ziara katika ofisi za Tume hiyo kubadilishana mawazo na uzoefu.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha-Rose Migiro, Naibu wake Ummy Mwalimu wakiwa katika picha ya kumbukumbu na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora jijini Dar es Salaam jana (Jumanne, Feb 24, 2015). Waziri alifanya ziara katika ofisi za Tume hiyo kubadilishana mawazo na uzoefu.
Picha na Farida Khalfan, Wizara ya Katiba na Sheria.
Na Martha Komba
Serikali imeiagiza Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHRGG) kuibua masuala yanayoathiri uzingatiaji wa haki za binadamu ili hatua stahiki zichukuliwe na hivyo kuboresha misingi ya haki na utawala bora nchini.
Akizungumza na viongozi wa Tume hiyo jana (Jumanne, Feb. 24, 2015) jijini Dar es Salaam, Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Asha–Rose Migiro alisema Serikali ina wajibu wa kuzingatia haki za binadamu katika utekelezaji wa majukumu yake na hivyo na hivyo ni muhimu kwa Tume kuibua na kutoa taarifa juu ya masuala ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...