Naibu Balozi wa Tanzania nchini Oman Juma Othaman (mwenye Kaunda suti) akipokea Tunzo ya ushiriki iliyotolewa na Mwakilishi kutoka Manispaa ya Mji wa Muscat ambao ni Waandaaji wa Maonesho ya Kimataifa ya Sanaa, Ubunifu na Utamaduni. Tanzania imepeleka zaidi ya Watu 40 kuonesha kazi wanazoifanya za sanaa ikiwemo,Uchongaji,uchoraji na ufumaji wa nguo. Kulia ni Kiongozi wa Msafara huo Khadija Battashy na kushoto ni Msaidizi kiongozi Masha Hussein. Picha na Faki Mjaka, Muscat Oman
Naibu Balozi wa Tanzania nchini Oman Juma Othman (katikati) akiwa kashika Tunzo ya ushiriki wa Maonesho ya Kimataifa ya Sanaa, Ubunifu na Utamaduni nchini Oman waliyopewa kutoka Manispaa ya Mji wa Muscat ambao ndio waandaaji wa Maonesho hayo. Kulia kwake ni Kiongozi wa Msafara wa Washiriki kutoka Tanzania Khadija Battashy na kushoto ni Msaidizi kiongozi Masha Hussein na Mkuu wa mambo ya kiufundi wa Msafara Moza Habib.

Na Faki Mjaka, Muscat Oman

Msemo wa Kiswahili usemao ‘aisifiaye Mvua huwa imemnyeshea’ unafanana kwa mbali na ule usemao ‘adhabu ya Kaburi aijuaye Maiti’. Misemo hii huonesha jinsi ambavyo muhusika kwenye tukio husika ndiye mwenye uelewa mpana zaidi wa kufahamu umuhimu au madhara ya jambo fulani.

Hata kunapotokea tatizo la kihalifu na kutakiwa ushahidi mara nyingi Polisi huanzia kuwakamata wale waliokuwa katika tukio hilo ili kusaidia kutoa ushahidi wa awali.

Mantiki ya utangulizo huo ni kusifia namna gani Ofisi ya Balozi wa Tanzania nchini Oman ilivyofanikisha Maonesho ya kimataifa ya Sanaa,Ubunifu na Utamaduni yanayofanyika nchini Omani na namna Maonesho hayo yanavyoweza kuisaidia Tanzania kupiga hatua mbele katika Sekta ya Kiutalii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...