Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Maendleo ya Jamii Bw. Xavier Keebwe akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa vijana kuhusu Sera ya maendeleo ya Vijana, Stadi za Maisha,Ujuzi, Mwongozo wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana yaliyotolewa na wawezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ambapo jumla ya zaidi ya Vijana 60 kutoka katika halmashauri za Manispaa ya Kigoma Ujiji, Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza na Kigoma Vijini mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbvi wa manispaa hiyo. Kutoka Kulia ni Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga na katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Mwezeshaji mkuu wa mafunzo hayo kutoka wizara hiyo Bibi. Esther Riwa.
Mtaalamu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Esther Riwa akitoa mada mbele ya Vijana kutoka Halmashauri za Manispaa ya Kigoma Ujiji, Wilaya ya Uvinza na Kigoma Vijijini katika warsha iliyofanyika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji.
Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akitoa mada mbele ya Vijana kutoka Halmashauri za Manispaa ya Kigoma Ujiji, Wilaya ya Uvinza na Kigoma Vijijini katika warsha iliyofanyika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji.
Baadhi ya Vijana wakifuatilia mada wakati wa warsha biliyoandaliwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa ajili ya kuhamasisha vijana kuhusu Mfuko wa maendeleo y Vijana nchini. Warsha hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji ambapo jumla ya zaidi ya vijana 60 kutoka katika halmashauri za Manispaa hiyo, Wilaya ya Uvinza na Kigoma Vijijini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...